Joseph Parker wa New Zealand ambaye ni mpinzani wa Anthony Joshua AJ katika pambano la masumbwi litakalofanyika siku ya jumamosi, amesema amejipanga kutumia akili nyingi, nguvu, na kasi kubwa ili kushinda.
Parker ambaye hajasikika akimzungumzia AJ ameweka wazi kuwa, yeye na timu yake walikuwa wakifanya mazoezi makali ili waweze kupata ushindi siku ya jumamosi.
Joseph Parker na AJ watakutanishwa tena na waandishi wa habari kuelekea pambano lao hilo litakalofanyika katika ukumbi ulioko kwenye uwanja principality mjini Cardiff.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |