Wapiganaji 20 wa kundi la Taliban wameuawa na wengine 13 kujeruhiwa baada ya jeshi la serikali ya Afghanistan kufanya operesheni mkoani Ghazni, mashariki mwa nchi hiyo.
Msemaji wa gavana wa mkoa huo Bw. Aref Nuri leo amesema, operesheni hiyo ilifanyika jana kwenye vijiji vya Khani Baba, Zaray na Dalil. Bw. Nuri pia amethibitisha vifo vya askari wawili na majeruhi watatu wa jeshi la serikali katika operesheni hiyo ambayo bado inaendelea.
Kundi la Taliban bado halijatoa tamko kuhusu ripoti hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |