Kocha mkuu wa timu ya Raga ya Uganda, Tolbert Onyango amesema kutokana na kiwango kilichoonyeshwa na timu yake kwenye mashindano ya Zimbabwe, ni wazi kuwa huenda wakapata matokeo mazuri kwenye mechi ya kufuzu kombe la dunia huko Hong Kong.
Timu ya Uganda inatarajiwa kuondoka jumapili hii kwenda Hong Kong ambako huko iko katika kundi E la mechi za kufuzu kombe la dunia pamoja na timu za Georgia, Japan na Chile.
Baada ya kumaliza mechi za kufuzu wiki ijayo Uganda watasafiri kwenda Australia ambako wanakabiliwa na michuano mingine ya Jumuiya ya madola.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |