Kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 80, mwaka huu katika mashindano ya kombe la dunia hakutakuwa na mwamuzi kutoka Uingereza, licha ya kuwepo majina yaliyopendekezwa.
Mark Clattenberg aliyechesha kwa mafanikio mechi ya fainali ya kombe la mataifa ya Ulaya, na ndiye aliyekuwa anapewa nafasi hiyo nchini Urusi mwaka huu, lakini kutokana nay eye kujiondoa katika waamuzi wa ligi kuu nchini Uingereza FIFA wakaondoa jina lake kwenye orodha ya waamuzi wake.
Chama cha soka cha Uingereza FA kiliiomba FIFA kuweka mbadala wake jambo ambalo halikuwezekana licha ya kupeleka majina ya wazoefu wakiwemo Martin Atkinson, Stuart Attwell, Robert Madley, Michael Oliver, Craig Pawson, Anthony Taylor na Paul Tierney.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |