Wajumbe wa Korea Kusini na Korea Kaskazini jana walifanya mazungumzo ya ngazi ya juu kwenye eneo salama la Panmunjom lililoko mpakani kati ya nchi hizo mbili, na kuamua kuwa viongozi wa nchi hizo mbili watakutana Aprili 27 kwenye eneo hilo. Pande hizo mbili pia zimeamua kufanya mazungumzo mengine Aprili nne kujadili maandalizi ya mkutano kati ya wakuu wa nchi hizo mbili.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |