Ikulu ya Palestina imelaani kauli alizotoa balozi wa Marekani nchini Israel Bw. David Friedman na kuzitaja kama uingiliaji wazi na usiokubalika wa mambo ya ndani ya Palestina. Taarifa iliyotolewa na msaidizi wa rais Abbas Bw. Nabil Abu Rudeineh inasema wapalestina hawatakubali uingiliaji wowote wa kigeni kuamua dhamira yao. Kabla ya hapo balozi wa Marekani nchini Israel Bw. David Friedman amesema kama rais Abbas hataki kufanya mazungumzo ya amani na upande wa Israel, Marekani itatafuta mtu mwingine wa kuchukua nafasi yake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |