Watu 23 wamejeruhiwa baada ya tetemeko la ardhi lenye nguvu ya 5.3 kwenye kipimo cha Richter kutikisa mkoa wa Kermanshah nchini Iran mapema jana. Mwezi Novemba mwaka jana tetemeko la ardhi lenye nguvu ya 7.3 lilikumba eneo hilohilo na kusababisha vifo vya watu 530 na wengine zaidi ya elfu nane kujeruhiwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |