Mashindano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na kati (CECAFA Club Cup) yanarejea tena mwaka huu baada kupumzika kwa kipindi cha miaka miwili kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ukosefu wa fedha za uendeshaji.
Kwa mwaka huu mashindano hayo yatafanyika nchini Tanzania, kuanzia June 30 hadi Julai 14, ambapo klabu za KCCA, GorMahia, Rayon Sports, Simba SC, AZAM FC, LLB, St George na El Hilal zinatarajia kupambana.
Mashindano hayo yanarejea kwa kile kilichodaiwa kuwa CECAFA imepokea fedha takribani dola za kimarekani milioni 1 kwa ajili ya kuendesha shughuli zake.
Bingwa wa mwisho katika mashindano ya klabu bingwa alikuwa Azam FC ilipoifunga Gor Mahia mwaka 2015.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |