Timu ya Menengai Homeboys ya mjini Nairobi imetwaa ubingwa wa ligi maalum ya raga kwa upande wa klabu nchini Kenya baada ya kuifunga Mwama RFC kwa alama 28-0 kwenye fainali iliyofanyika mjini Nakuru.
Homeboys ambao ni kwa mara ya pili mfululizo wanashinda taji, walifanikiwa kufuzu hatua ya nusu fainali kwa kuwashinda Menengai Oilers kwenye nusu fainali kwa alama 29-5.
Kwa upande wao Mwamba walifuzu fainali kwa kuwafunga Kabras Sugar kwa alama 17-12 kwenye mchezo wao wa fainali uliofanyika siku ya jumamosi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |