• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Umoja wa Afrika wathibitisha vifo vya wapiganaji 30 wa Al Shabaab katika mapambano kusini mwa Somalia

    (GMT+08:00) 2018-04-02 18:39:33

    Kikosi cha Kulina Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) kimethibitisha kuwa watu 34 wameuawa wakati wa mapigano makali kati ya kikosi hicho na wapiganaji wa kundi la Al Shabaab kusimi mwa Somalia hapo jana.

    Mwakilishi maalum wa mwenyekiti wa kamati ya Umoja wa Afrika kuhusu Somalia, Fransisco Madeira amesema, wapiganaji 30 wameuawa baada ya vikosi vya Umoja huo kuzuia magaidi walioshambulia kambi ya kikosi hicho mkoani Lower Shabelle. Madeira amesema, askari wanne wa AMISOM waliuawa katika mapigano hayo huku wengine sita wakijeruhiwa.

    Hata hivyo, kundi la Al Shabaab linadai kuwa wapiganaji wake wamewaua askari 59 wa Uganda katika mapigano hayo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako