KATIBU Mkuu Wizara ya Michezo ya Zanzibar Omar Hassan Omar, ametangaza kuwa Wizara yake imejipangia mwongozo wa kuifanya Sekta ya michezo iinue uchumi mkubwa kwa vijana.
Alisema kuwa ili kufikia malengo hayo ni lazima pawepo na ushirikiano mkubwa kutoka kwa asasi zingine za kiserikali na zisizo za kiserikali akitolea mfano Wizara ya Elimu ambayo ameiomba kuzingatia suala la uimara wa masomo ya michezo na utamaduni.
Mfano mzuri akiutoa wakati wa ufunguzi wa mashindano ya kitaifa ya Sanaa ya Maigizo na Uchoraji, ambayo yatafanyika kwa muda wa miezi mitatu katika ngazi ya shule.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |