Michuano ya soka ya klabu bingwa barani ulaya inarejea leo kwa mechi mbili za kwanza za hatua ya robo fainali zitakazopigwa katika miji ya Turin nchini Italia na Seville nchini Hispania.
Nchini Italia, wenyeji Juventus watawakaribisha Real Madrid kutoka Hispania majira ya saa tatu za usiku kwa saa za Afrika Mashariki.
Kwingineno katika muda huo huo nchini Hispania, Sevilla FC itakuwa katika uwanja wake wa nyumbani kucheza Bayern Munich ya Ujerumani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |