Waraka rasmi uliotolewa na Ofisi ya Habari ya Baraza la Serikali la China umeonyesha kuwa China ina waumini milioni 200 wa dini mbalimbali na viongozi karibu laki 380.
Waraka huo unaoitwa "Sera na Hatua za China katika Kulinda Uhuru wa Kuabudu" umebainisha kuwa, dini kubwa zinazofuatwa nchini humo ni Ubuddha, Taoism, Uislam, Katoliki, na Protestanti.
Waraka huo pia umesema kuna makundi 5,500 ya kidini nchini China yakiwemo saba ya kitaifa ambayo ni pamoja na Jumuiya ya Buddha ya China, Jumuiya ya Waislam wa China, na Baraza la Kikristo la China.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |