Tume ya Umoja wa Mataifa ya kuondoa mabomu ya ardhini (UNMAS) leo imesema raia wasiopungua elfu 3 wa Somalia wameuawa au kujeruhiwa na mabomu katika miaka 3 iliyopita.
Tume hiyo imesema, mwaka jana, hali nchini Somalia ilikuwa mbaya zaidi, ambapo shambulizi kubwa la mabomu lilitokea tarehe 14 mwezi Oktoba huko Mogadishu na kusababisha vifo vya watu wasiopungua 500 na wengine zaidi 300 wamejeruhiwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |