Uongozi wa klabu ya Yanga kupitia Afisa Habari wake, Dismas Ten, umewaomba mashabiki na wanachama wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi katika mchezo wa kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Welayta Dicha FC mchezo utakaopigwa Jumamosi uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Yanga itakuwa ina kibarua hicho cha mkondo wa kwanza baada ya kuondoshwa ligi ya mabingwa Afrika dhidi ya Township Rollers ya Botswana.