Mahakama kuu ya mjini Durban nchini Afrika Kusini imetangaza kuahirisha kesi ya ufisadi inayomkabili Rais wa zamani wa nchi Bw. Jacob Zuma hadi Juni 8 mwaka huu.
Jopo la wanasheria wa serikali na mawakili wa utetezi wamekubaliana kutoa ombi la kuahirishwa kwa shauri hilo hadi Juni 8, ambalo lililokuja dakika chache baada ya Bw. Zuma kuwasili mahakamani hapo kujibu mashtaka 16 ya matumizi mabaya ya fedha, rushwa na kujipatia pesa kwa njia zisizo halali.
Kulikuwa na hali ya furaha miongoni mwa mamia ya wafuasi wa Zuma waliokusanyika nje ya mahakamni hiyo, ambao walishangilia kufuatia tangazo la kesi kuahirishwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |