Akishiriki kwenye mkutano wa 32 wa baraza la kikanda la kupambana na ugaidi la Jumuiya ya Ushirikiano wa Shanghai(SCO) mjini Tashkent, nchini Uzbekistan, Bw. Smirnov amesema, wapiganaji hao wakiwemo wa kundi la IS, ni tishio la usalama kwa nchi wanachama wa SCO. Nchi hizo zimeamua kushirikiana kwa pamoja na kuchukua hatua kupunguza tishio hilo kadiri ziwezavyo, ambazo ni kubadilishana habari za wapiganaji na kuzuia wapiganaji hao kuingia kwenye nchi hizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |