Shirika la nishati ya atomiki la Iran limesema kinu kimoja cha nyuklia kilichoko mjini Teheran kimekarabatiwa upya na kuanza kufanya kazi. Mkurugenzi wa shirika hilo amesema ukarabati wa kinu hicho cha nyuklia kilichotumika kwa miaka 40, unalenga kukifanya kiwe cha kisasa. Ofisa huyo amepongeza mafanikio yaliyopatikana na watafiti wa Iran, na kusema hivi sasa Iran imepata maendeleo makubwa kwenye matumizi ya nishati ya nyuklia kwa njia ya amani, na inaweza kutengeneza vifaa vingi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |