Waziri wa ulinzi wa Israel Bw. Avigdor Lieberman ametoa wito wa kufanyika wa uchunguzi dhidi ya Shirika la haki za binadamu la Israel B'Tselem, ambalo lilifanya kampeni ya kuwataka askari wakatae kutii amri ya kuwafyatulia risasi waandamanaji wa Palestina kwenye ukanda wa Gaza. Bw. Lieberman amesema shirika hilo linalohujumu nchi liko pamoja na wale wanaoichukia Israel na wale wanaowashutumu askari wa Israel kuchukua hatua kinyume cha sheria, na amemtaka mwanasheria mkuu wa Israel kuanzisha uchunguzi dhidi ya viongozi wa shirika hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |