• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Msemaji wa serikali ya Uganda asema kitendo cha kuipaka matope China hakitafanikiwa

    (GMT+08:00) 2018-04-09 09:26:09

    Msemaji wa Serikali ya Uganda Bw. Ofwono Opondo ametoa makala kwenye gazeti kubwa la nchi hiyo the New Vision akisema, kitendo cha kuipaka matope China hakitafanikiwa.

    Kwenye makala hiyo Bw. Opondo amesema rais Donald Trump wa Marekani amekuwa akiongea mara nyingi kwenye ukurasa wake wa Twitter kwamba mgogoro wa kibiashara utaleta faida, na Marekani itashinda kwenye mgogoro huo kwa urahisi. Lakini hajui kuwa muundo wa dunia umebadilika kwa kiasi kikubwa.

    Amesema ingawa Marekani inadumisha hadhi yake kuwa nchi yenye nguvu kubwa zaidi duniani, lakini tabia yake ya ujeuri haikubaliki.

    Pia amesema jaribio lake la kuipaka matope China halitakuwa na mafanikio, kwa sababu ustawi wa China na ushiriki wake kwenye mambo ya kimataifa vimeleta utulivu wa kisiasa, usalama wa kijamii na maendeleo ya kiuchumi kwa nchi zote duniani zikiwemo nchi za Afrika. Pia anaona ni jambo zuri kwa Serikali ya China kutangaza kuchukua hatua za kujibu hatua ya Marekani kutoza ushuru wa forodha dhidi ya bidhaa za China.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako