Mkutano wa mwaka 2018 wa baraza la Asia la Bo'ao umefunguliwa mkoani Hainan China. Rais Xi Jinping wa China ametoa hotuba kwenye ufunguzi wa mkutano huo.
Rais Xi ametoa ufafanuzi kuhusu jinsi China itakavyohimiza ufunguaji mlango na kuimarisha mageuzi, na kueleza msimamo wa China kuhusu kujenga mustakabali wa pamoja wa Asia na binadamu, na kuanzisha mustakabali mzuri wa Asia na Dunia.
Wageni zaidi ya 2000 kutoka sehemu mbalimbali duniani wanahudhuria mkutano huo, wenye kauli mbiu ya "Asia inayofungua mlango na yenye uvumbuzi kwa ajili ya dunia yenye ustawi na maendeleo"
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |