Timu ya Rwanda ya mpira wa wavu kwa viwanja vya ufukweni 'beach volleyball' jana imefuzu hatua ya robo fainali kwenye michezo ya jumuiya ya madola inayoendelea nchini Australia baada ya kuishinda timu ya Singapore.
Rwanda inayoundwa na Denise Mutatsimpundu and Charlotte Nzayisenga iliishinda Singapore kwa seti ya 2-0 licha ya Kukabiliwa na upinzani mkali.
Kwa matokeo hayo timu ya Rwanda inafuzu kwa kuwa washindi wa watatu kwenye kundi C la mashindano hayo nyuma ya New Zealand inayoongoza na Vanuatu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |