Rais Xi Jinping wa China leo amesema, tangu miaka mitano iliyopita alipotoa pendekezo la "Ukanda Mmoja na Njia Moja", nchi na mashirika ya kimataifa zaidi 80 zimesaini makubaliano ya ushirikiano wa "Ukanda Mmoja na Njia Moja". Katika ujenzi wa "Ukanda Mmoja na Njia Moja", China haitafanya mashindano ya kijiografia, haitajenga maeneo yake ya kupinga pande yoyote, haitalazimisha pande nyingine. Pande mbalimbali zinapaswa kushikilia na kufuata kanuni za kujenga kwa pamoja na kunufaisha kwa pamoja, na kujenga "Ukanda Mmoja na Njia Moja" kuwa jukwaa la ushirikiano wa kimataifa linalofuata mkondo wa utandawazi wa uchumi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |