Mkurugenzi mkuu wa Chai anazingatia kufanya uchunguzi ili kupata sababu za msingi zinazoathiri thamani ya bidhaa.
Katika kipindi cha wiki sita, bei imeshuka katika mnada wa Mombasa, jambo ambalo limetia wasiwasi wadau na kuelezea mapato duni ya wakulima mwaka huu.
Mkuu wa bodi Samuel Ogola anasema ingawa bei imeathiriwa na ongezeko la kiasi, kunaweza kuwa na mambo mengine.
Katika uuzaji uliofanyika juma jana, kilo ilikuwa inauuzwa Sh260, chini ya Sh262 katika mnada uliopita.
Kenya ndio muuzji mkuu wa chai nyeusi duniani na inachangia asilimia 24 ya ya mauzo ya kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |