Jeshi la Nigeria limethibitisha kuwa vikosi vyake vimekamata mshukiwa wa ugaidi mwenye utaalamu wa kutengeneza mabomu ya kienyeji kwa ajili ya kundi la kigaidi la Boko Haram. Msemaji wa jeshi hilo Bw. Onyema Nwachukwu amesema mshukiwa huyo anayetambulika kwa jina la Adamu Hassan alikamatiwa katika jimbo la Gombe lililoko kaskazini mashariki mwa nchi hiyo, kufuatia operesheni ya pamoja ya jeshi na polisi wa siri iliyofanyika jumatatu. Msemaji huyo pia amesema mshukiwa huyo amekiri makosa kwa mamlaka ya usalama.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |