Baraza la usalama la Umoja wa mataifa limepitisha uamuzi wa kurefusha muda wa idhini ya Tume ya Umoja wa mataifa ya Misaada ya kisheria nchini Haiti kwa mwaka mmoja zaidi, hadi Aprili 15 mwaka kesho. Kwa mujibu wa uamuzi huo, tume hiyo iliyoanza kutekeleza majukumu yake mwezi Oktoba mwaka jana kuimarisha taasisi za kisheria na kuunga mkono polisi wa Haiti, inaweza kupunguza idadi ya maofisa wake wa polisi kuanzia mwezi Oktoba mwaka huu endapo hali ya usalama itaboreka.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |