• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Jeshi la Israel latangaza matokeo ya awali ya uchunguzi kuhusu mdunguaji kumpiga risasi mpalestina

    (GMT+08:00) 2018-04-11 09:25:33
    Msemaji wa jeshi la Israel tarehe 10 ametoa taarifa akitangaza matokeo ya awali ya uchunguzi kuhusu mdunguzi kumpiga risasi mpalestina, na kukitaja kitendo hicho kuwa "mbinu ya mwisho baada ya kushindwa kuwatawanya wapelstina kwa njia zisizo za kuwaua".

    Juzi video kuhusu mdunguaji wa jeshi la Israel kumfyatulia risasi mpalestina ilisambaa kwenye mtandao wa Internet, ikionyesha mdunguaji mmoja akimfyatulia risasi mpalestina aliyekuwa karibu na uzio wa mpaka kati ya Israel na Gaza, , na askari wa jeshi la Israel waliokuwepo walionekana kushangilia baada ya kuona mpalestina huyo akianguka kutokana na kujeruhiwa na risasi.

    Msemaji wa jeshi la Israel amesema video hiyo ilipigwa mwezi Desemba mwaka jana kwenye ukanda wa Gaza. Askari hao kwenye video wataadhibiwa, na jeshi la Israel litachunguza tukio hilo kwa pande zote.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako