Viongozi wa wilaya ya Pakwach nchini Uganda wameelezea kusikitishwa kwao na kupungua kwa samaki aina ya Alestes Baremose maarufu kama Angara.
Aina hiyo ya samaki ina protini za juu na hupendwa na watu wa Kaskazini mwa Uganda na wanapatikana katika ziwa Albert.
Maafisa wamelaumu utumiaji wa vifaa duni za kuvua na uvuaji samaki kupita kiasi kama moja ya sababu zinazotishia kuangamia kwa samaki hao.
Mwenyekiti wa wilaya hiyo Robert Osteen Omito, amesema pia samaki hao ni kitega uchumi kwa watu wnaaoishi kwenye eneo hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |