Muungano wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia umesema vikosi vya ulinzi wa anga vya Saudi Arabia vimefanikiwa kuzuia makombora mawili yaliyorushwa na kundi la Houthi kutoka nchini Yemen, na kutungua ndege mbili zisizo na rubani za kundi hilo. Saudi Arabia imeshuhudia mashambulizi mengi ya makombora yanayorushwa na kundi la Houthi, baada ya nchi hiyo na washirika wake kuanzisha operesheni za kijeshi za kupambana na kundi hilo mwezi Machi mwaka 2015.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |