Baada ya Marekani kuchukua hatua za kuchochea mgogoro wa kibiashara dhidi ya China, wachambuzi wa nchi mbalimbali wanaona vitendo hivyo vya Marekani vinaonesha kutojiamini, na vitaharibu mfumo wa biashara ya pande nyingi.
Mhadhiri wa uchumi katika Chuo Kikuu cha Kenyatta cha Kenya Bw. Ken Ogenbo anaona hatua zilizochukuliwa na China kujibu vitendo vya Marekani ni thabiti na za kujizuia.
Aliyekuwa balozi mdogo wa uchumi wa Afrika Kusini nchini China Bw. Yusufu Adam amesema, hatua za upande mmoja za Marekani zitaweza kuweka hatarini uchumi wa dunia. Amesisitiza kuwa nchi nyingine hazipaswi kukaa kimya, na zinatakiwa kuchukua hatua za kujibu mapema.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |