• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda:Rais Kagame afanya mabadaliko katika baraza la mawaziri

    (GMT+08:00) 2018-04-12 19:47:49

    Rais wa Rwanda Paul Kagame amefanya mabadiliko katika baraza la mawaziri .

    Uzziel Ndagijimana ameteuliwa kuwa waziri mpya wa fedha akichukua nafasi ya Claver Gatete aliyejitahidi kustawisha thamani ya sarafu ya nchi hiyo wakati alipoongoza wizara hiyo.

    Sasa Gatete amehamishwa hadi wizara ya miundo msingi .

    Kagame analenga kuimarisha sekta ya teknolojia ,madini,utalii na kilimo anazosema zitaimarisha pakubwa kasi ya maendeleo ya uchumi wan chi hiyo.

    Shirika la fedha la kimataifa IMF linatarajia uchumi wa Rwanda kukuwa kwa asilimia 7,2 mwaka huu kutokana na miradi mikubwa maendeleo iliyobuniwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako