Rais Xi Jinping ametuma salamu za pole kwa mwenzake wa Algeria Bw. Abdelaziz Bouteflika kutokana na ajali ya ndege ya jeshi iliyotokea hivi karibuni nchini Algeria.
Katika salamu hizo, rais Xi amesema kwa niaba ya serikali na watu wa China pamoja na yeye binafsi, anatoa salamu za rambirambi kwa familia za wafiwa na kutoa salamu za pole kwa majeruhi katika ajali hiyo.
Waziri mkuu wa China Bw. Li Keqiang pia ametoa salamu za pole kwa mwenzake wa Algeria Bw. Ahmed Ouyahia kutokana na ajali hiyo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |