Waziri wa mambo ya nje wa Russia Bw. Sergei Lavrov amesema kuwa taarifa ilizopata Russia kwa njia ya siri zinaonesha kuwa sampuli za sumu aliyowekewa jasusi wa zamani wa Russia nchini Uingereza ambazo zilikusanywa na Shirika la kupiga marufuku silaha za kikemikali OPCW, zina sumu iliyoendelezwa na NATO aina ya BZ. Bw. Lavrov amesema Urusi na Russia hazikuwahi kutafiti wala kuhifadhi sumu ya aina hiyo, na pia ameeleza mashaka yake kuhusu OPCW kupuuza uwepo wa sumu ya BZ kwenye ripoti yake ya uchunguzi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |