Nchi ya Rwanda inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano mkuu wa mwaka wa shirikisho la vyama vya mchezo wa tennis Afrika utakaofanyika Aprili 27 na Aprili 28.
Taarifa hiyo imetolewa na Rais wa Chama cha Tennis cha Rwanda RTF, imeeleza kuwa viongozi kadhaa kutoka nchi 50 ambazo ni wanachama pamoja na viongozi kutoka chama cha tennis duniani ITF watahudhuria.
Hii ni mara ya kwanza kwa Rwanda kuandaa mkutano huo na ikiwa ni kwa mara ya kwanza unafanyika nje ya nchi zilizozoeleka za Morocco, Algeria, Egypt au South Africa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |