Dereva wa timu ya Mercedes, Daniel Ricciardo raia wa Australia, jana ameshinda taji la China la mashindano ya magari ya mwendokasi, yaliyofanyika jana mjini Shanghai.
Huu ni ushindi wa sita kwa Ricciardo tangu aanze kushiriki mashindano hayo mwaka 2011 na akiwa tayari ameshiriki mara 132.
Madereva wengine ambao wanawania ubingwa wa jumla msimu huu, Lewis Hamilton wa Uingereza na Sebastian vettel jana walishindwa kumaliza katika nafasi tatu za juu kwa zilitwaliwa na Valterri Botas wa timu ya Mercedes pamoja na Kimi Raikonnen wa Ferari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |