Pande mbalimbali nchini Palestina zimepongeza kupitishwa kwa azimio kuhusu suala la Palestina kwenye Mkutano wa kilele wa nchi za kiarabu. Waziri wa mambo ya nje wa Palestina Riyad Malik amesema mkutano huo umepitisha mapendekezo yote yaliyowasilishwa na Palestina, hali ambayo inaonesha uungaji mkono wa nchi za kiarabu kwa watu wa Palestina na haki zao halali. Azimio lililopitishwa kwenye mkutano huo linatambua Jerusalem Mashariki kuwa sehemu isiyotengeka ya ardhi ya Palestina, na kupinga kithabiti uamuzi wa Marekani kutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel na kuutaja kuwa ni batili na unakiuka sheria za kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |