Mwanamasumbwi Anthony Joshua wa Uingereza, kwa mara ya kwanza amejibu kauli za mabondia wanaomhasimu, Deontay Wilder wa Marekani na Tyson Fury wa Uingereza.
Katika maneno yake kwa waandishi wa Habari bingwa huyo wa mikanda mikubwa mitatu ya IBF, WBO na WBA amesema anaamini katika uwezo wake hivyo yuko tayari kupigana nao wote wawili.
Lakini kwanza amesema atapigana na Wilder ili kuchukua mkanda wa WBC andipo atarudi kupigana na Tyson ambaye ametangaza kurejea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |