Msemaji wa jeshi la Somalia Bw. Mohamed Noor Agajof amesema vikosi vya serikali vimewaua wapiganaji 30 wa kundi la Al-Shabaab kwenye operesheni iliyofanyika mkoani Hiiraan, katikati ya Somalia .
Msemaji huyo amesema baada ya mapambano makali, vikosi vya serikali vimedhibiti vituo vya wapiganaji, na kukamata silaha na vifaa vyao.
Hivi karibuni jeshi la serikali ya Somalia limeimarisha mapambano dhidi ya kundi la Al-Shabaab chini ya uungaji mkono wa Tume ya Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |