Wafuatiliaji wa amani nchini Sudan Kusini wamesema mazungumzo yajayo ya amani yaliyopangwa kufanyika tarehe 26 Aprili yameahirishwa hadi itakapotolewa taarifa zaidi.
Tume ya Ufuatiliaji na Tathmini (JMEC) imesema tarehe mpya ya mazungumzo hayo itatangazwa na mwenyekiti wa baraza la mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo ya Kiserikali ya Nchi za Afrika Mashariki IGAD .
Kwa mujibu wa habari kuahirishwa huko kutatoa nafasi ya mazungumzo yenye ufanisi kwa wadau mbalimbali husika.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |