Timu mpya ya taifa ya Rwanda ya mchezo wa jadi wa kupigana kwa kutumia mapanga marefu (chanbara) itashiriki kwa mara ya kwanza katika mashindano ya Dunia yatakayofanyika mwezi Disemba mwaka huu mjini Tokyo.
Kwa mujibu wa kiongozi wa shirikisho la mchezo huo nchini Rwanda, Benjamini Nyirimbabazi, timu ya Rwanda itakuwa na wachezaji wawili ambao watateuliwa kutokana na wachezaji wanaojiandaa.
Chanbara iliasisiwa nchini Rwanda mwaka 2013, na mkufunzi kutoka Japan aitwaeTsutomu Takahashi, na Nyirimbazi ndiye mchezaji wa daraja la juu kabisa mwenye mkanda mweusi (black belt)
Kwa nchini Rwanda, chanbara ni mchezo mpya na malengo yaliyowekwa ni kuuendeleza ili ufikie viwango vya kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |