• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Jeshi la Somalia laua wapiganaji kadhaa wa Al-Shabab kusini mwa nchi hiyo

    (GMT+08:00) 2018-04-18 20:41:01

    Wapiganaji kadhaa wa kundi la Al-shabab wameuawa na wengine kujeruhiwa katika mapigano na jeshi la Somalia SNA likishirikiana na kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika katika eneo la Qoqani, jimbo la Lower Jubba kusini mwa Somalia.

    Ofisa mmoja wa jeshi katika eneo hilo Hassan Aden Mohamed amesema, wapiganaji wa Al-Shabab walishambulia kituo cha jeshi kilichoko Qoqani mkoani humo, ambapo jeshi la serikali ya Somalia lilipambana nao. Hakuna vifo na majeruhi kwa jeshi la Somalia na askari wa AMISOM.

    Lakini wapiganaji wa Al-Shabab wametangaza kushinda katika mapambano hayo, na kusema wamedhibiti kambi kadhaa za jeshi la Somalia katika eneo hilo na kuwaua askari kadhaa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako