Mkutano wa Baraza la kimataifa la kuhimiza ushirikiano kati ya China, Japan na Korea Kusini umefanyika jana mjini Tokyo. Akihutubia ufunguzi wa mkutano huo Katibu mkuu wa sekritarieti ya ushirikiano kati ya China, Japan na Korea Kusini TCS Bw. Lee Jong-heon amesema kuimarisha ushirikiano ni matarajio ya muda mrefu ya nchi hizo tatu, na zinapaswa kuendelea na juhudi za kuimarisha uhusiano na ushirikiano kati yao kwa njia ya kuimarisha mawasiliano na maelewano. Mkutano huo ulioandaliwa na TCS na wenye kauli mbiu "Kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano kati ya nchi tatu" ulihudhuriwa na watu zaidi ya 300 kutoka sekta mbalimbali za nchi hizo tatu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |