Wizara ya mambo ya nje ya Syria imesema, kikosi kazi cha uchunguzi cha Shirika la kupiga marufuku silaha za kikemikali OPCW kimewasili mjini Douma, mashariki mwa Damascus, Syria, ili kutathmini hali ya usalama ya huko.
Naibu waziri wa mambo ya nje wa Syria Bw. Faisal Mekdad amesema, serikali ya Syria itaunga mkono uchunguzi wa OPCW. Pia amesema ujumbe huo umefanya mazungumzo mara nyingi na serikali ya Syria kuhusu kufanya uchunguzi kwa haki, uwazi na usahihi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |