MKUTANO wa wadau na wawekezaji wa pamba, kutoka mikoa 17 inayozalisha zao hilo wameweka maazimio 10 ya kuboresha mnyororo wa zao hilo kuanzia kwa mkulima mzalishaji, mchakataji hadi mtengenezaji nguo nchini.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Profesa Elisante ole Gabriel mjini Dodoma amesema, serikali ipo tayari kushirikiana nao, ili wapate mafanikio makubwa.
Aidha, amesema wizara hiyo itaunda Kamati Maalumu itakayoshirikisha vijana wenye taaluma kutoka katika wizara hiyo ili kujifunza kutoka kwa wazee wazoefu waliopo katika sekta binafsi na hata kutembelea China kujifunza mifumo mbalimbali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |