Afisa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo, amesema kuwa jumla ya Camera 109 zitafungwa Uwanjani kuelekea mechi hiyo inayoteka hisia za mashabiki na wadau wa soka nchini Tanzania na Afrika Mashariki.
Clifford ameeleza kuwa Camera hizo zitafungwa ili kuimarisha ulinzi na usalama ndani ya uwanja ambapo zitakuwa zinarekodi matukio mbalimbali kabla na baada ya mchezo.
Mechi hiyo inatarajiwa kupigwa Aprili 29 uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |