Kuna msemo usemao "Kutangulia si kufika, na wengine husema "ujanja kupata si kuwahi" misemo hii miwili inawahusu Bayern Munich baada ya kutangulia kufunga goli kupitia kwa Josh Kimmich katika dakika ya 28 ya mchezo kabla ya Marcelo kuisawazishia Real Madrid dakika ya 44.
Marco Asensio alishindilia msumari wa mwisho kwa Bayern Munich baada ya kuipatia timu yake Real Madrid goli la ushindi katika dakika ya 57.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |