Rais Xi Jinping wa China na waziri mkuu wa India Bw. Narendra Modi ambaye yuko ziarani nchini China wamefanya mkutano usio rasmi huko Wuhan, katikati ya China.
Mkutano huo kati ya viongozi hao wawili ulianza kutoka jumba la makumbusho la mkoa wa Wuhan. Viongozi hao waliangalia utamaduni wa China wenye historia ndefu, huku wakibadilishana maoni kuhusu kuimarisha mawasiliano kati ya nchi hizo mbili na kuhimiza kuishi kwa amani kwa tamaduni tofauti. Baada ya hapo, viongozi hao walifanya mazungumzo kwenye hoteli ya Donghu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |