Madaktari zaidi ya 600 wa kujitolea leo wamefanya kumbukumbu ya miaka 10 tangu kutokea kwa tetemeko kubwa la ardhi la Wenchuan tarehe 12, Mei mwaka 2008, ambapo watu takriban elfu 70 walifariki.
Madaktari hao kutoka Beijing na sehemu nyingine nchini China wamekusanyika katika shule ya sekondari ya Xuankou ya wilaya ya Wenchuan mkoani Sichuan, na kuwakumbuka watu waliofariki kwenye tetemeko hilo. Baadaye walitembelea maonesho ya picha ya kumbukumbu ya miaka 10 tangu kutokea kwa tetemeko hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |