Kampuni moja ya Uingereza inayouza chai ya Kenya itaonyesha bidhaa hiyo kwenye maonyesho ya chai ya Ulaya mjini London kuanzia tarehe 22 hadi 23 mwezi huu.
Kampuni hiyo Kenya Tea inaagizia chai ya Kenya moja kwa moja kutoka kwa wakulima na baadaye kuuza kote duniani.
Kwa sasa Kenya iko kwenye nafasi ya tatu miongoni mwa nchi zinazozalisha chai kwa wingi ikiwa nyuma ya China na India.
Uingereza ndio mnunuaji wa tatu mkuu wa Chai ya Kenya, nchi nyingine zikiwa ni Pakistan na Misri.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |