Mradi wa franc bilioni 22 ambayo itajengwa katika wilaya nne.
Meneja wa Idara ya Mipango katika Shirika la Maendeleo la Usafiri Rwanda (RTDA), Fabrice Barisanga, amesema ujenzi utaanza mwishoni mwa mwaka 2018 na utakamilika mwisho wa 2019, na kuanza kutumiwa mwaka wa 2020.
Aidha amesema kutakuwa na abiria zaidi wakitumia usafiri wa bahari kwa sababu itakuwa nafuu zaidi kuliko usafiri wa barabara.
Makampuni mengine ambayo yanaweza kufaidika kwa kutumia vituo ni pamoja na BRALIRWA mzalishaji wa saruji, CIMERWA, viwanda vya chai na makampuni ya kahawa katika Mkoa wa Magharibi.
Bandari, itaongeza biashara ya mpakani kama watu wengi wanatoka DR Congo kununua bidhaa kutoka masoko makubwa katika Rubavu na Karongi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |